Thursday, 30 October 2014

ajivunia kuwa shoga asema mkuu wa Apple

                                              Mkuu wa kampuni ya Apple Tim Cook
Mkuu wa kampuni ya Apple Tim Cook ametangaza jinsia yake akisema kuwa ''anajivunia kuwa shoga''..
Bwana Cook alitoa tamko hilo ili kujaribu kuwasaidia watu wanaong'ang'ana kutangaza jinsia zao katika ripoti iliochapishwa katika gazeti la biashara la kila wiki la Bloomberg.
Amekuwa wazi kuhusu jinsia yake,lakini pia amejaribu kuweka maisha yake katika faragha hadi sasa alisema.
 
 
Nembo ya kampuni ya Apple
Wiki hii Bwana Cook alitoa changamoto kwa jimbo lake la Alabama kuhakikisha kuwa haki za mashoga na wale wanaobadili jinsia zinaheshimiwa.
''Mimi sijitambui kama mwanaharakati,lakini nimegundua nilivyofaidika na mikakati iliowekwa na wengine'',alisema bwana Cook.
''Kwa hivyo iwapo watu wakisikia kwamba mimi ni shoga kutawasaidia baadhi yao ,ama kumpa faraja yule anayejisikia mpweke ama kuwashinikiza wengine kupigania haki zao,basi afadhali kutangaza maisha yangu ya faragha''aliongezea.
Bwana Cook amesema amekuwa wazi kuhusu jinsia yake na watu wengi wakiwemo wafanyikazi wenzake katika kampuni ya Apple,lakini hilo halikuwa chaguo rahisi kutangaza hadharani kuhusu jinsia yake.

Rihanna Ayaanika Maungo Yake




 Rihanna Nia Mwanamuziki Asieishiwa Vituko Kila Kukicha Lazima Awe Na Kituko Kipya Na Kuaacha Mashabiki Wake Hoi Kivazi Alichokivaa Rihanna Katika Inspiration Gala Nchini Marekani Katika Kitongoji Cha Los Angeles Katika Hafla  Hiyo Alionekana  Tofauti Na Hafla Zilizopita Angalia Picha Zake Hapo Chini.






Picha 3 za jinsi Waziri mkuu wa Uganda alivyonyang’anywa ulinzi nyumbani baada ya kutimuliwa kazi.




ug1Jana ndio Waziri mkuu mpya wa Uganda Ruhakana Rugunda kaapishwa ila kabla yake alikua ni Amama Mbabazi ambae alifutwa kazi wiki kadhaa zilizopita baada ya kukaa madarakani toka May 2011 akitokea kwenye Uwaziri wa Ulinzi.
September 18 2014 ndio Rais Museveni alimuandikia Spika wa bunge barua kumuarifu kuwa ameamua kumuondoa waziri mkuu huyo na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekua Waziri wa Afya ambae kwa sasa ana umri wa miaka 67.
ug2
Kwa mujibu wa ripota wa TZA (millardayo.com na AyoTV) waziri huyu alietimuliwa alikua Waziri mkuu wa nne toka Rais Museveni aanze kuitawala nchi hiyo January 1986 ambapo mpaka sasa amewahi kuwa na Makamu wa Rais wanaofikia wanne.
Picha zote hizi zinaonyesha wakati Serikali ya Uganda ilipomnyang’anya ulinzi wa Wanajeshi waziri huyu mkuu baada ya kufutwa kazi ambapo kwenye hii picha ya chini anaeonekana ni mke wake akilalamika kwa kutoamini kilichotokea kwani mume wake na Rais Museveni wamekua marafiki wakubwa.
Vyombo mbalimbali vya habari vimeripoti kwamba kuna mambo mengi yaliyosababisha kufutwa kazi kwa waziri huyu mkuu lakini mambo hayo hayajawekwa wazi.
ug3
Nyuma hii unayoiona ni nyumba anayoishi na inayomilikiwa na Waziri huyu mkuu aliefutwa kazi.
Unataka niwe nakusogezea kila stori inayonifikia zikiwemo pichaz, video’s na stori zenyewe? niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook cha kufanya ni kujiunga na mimi kwa kubonyeza >>> twitter Insta Facebook

Na Mkubwa Fella kaingia kwenye siasa… unachotakiwa kufahamu kwa sasa kiko hapa



fella_l
Listi ya mastaa au watu maarufu wa Tanzania ambao wametangaza kujiingiza kwenye siasa imezidi kuongezeka ambapo leo boss wa kundi la TMK Wanaume Said Fella, ametangaza kwa mara ya kwanza nia yake ya kujiingiza katika siasa na kwa sasa amevaa Gwanda la kugombea nafasi ya uongozi kwenye serikali ya mtaa Kirungule kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katika ukurasa wake wa Instagram (@mkubwafella) ameomba watu wake waungane nae kwenye hili pia ili aweze kuichukua hiyo nafasi kwa kuandika ‘Leo wadau naomba dua zenu nagombea serikali ya mtaa huku kwetu Kitungule na nipo na Mgombea mwenzangu ndio tunagombania hiki kiti apate yeye au nibebe mimi Inshaallah’
Mkubwa FellaMkubwa Fella II
Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza >>> twitter Insta Facebook

Picha 4 za Chidi Benz baada ya kupata dhamana Mahakamani leo.


Heo.chidi 3 
Alishikiliwa na Polisi baada ya kukutwa na dawa za kulevya kwenye uwanja wa ndege Dar es salaam wakati akijiandaa kupanda ndege kwenda Mbeya kwenye show.
Baada ya kufikishwa Mahakamani October 28 2014 na kusomewa mashtaka matatu alirudishwa rumande huku kesi yake ikiahirishwa mpaka November 11 2014 na wakati huohuo pia ikisemekana alikua kwenye mipango ya kupata dhamana.
October 29 2014 Chidi Benz alipata dhamana kwenye Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu baada ya kupata Wadhamini wawili pamoja na shilingi milioni moja.
chidi 4
Chidi 2
Chidi 1

Hawa ndio mastaa wanaogombea Ubunge jimbo moja kupitia vyama tofauti.



Red CarpetTaarifa kuhusiana na mastaa mbali mbali ikiwemo wa muziki, filamu, na michezo kuingia katika headline zinazowazungumzia kujihusisha na siasa sio taarifa ngeni kuzisikia, ambapo kwa sasa mastaa wa movie wanaingia kwenye headline nyingine ya wao kwa wao kugombea nafasi ya ubunge kwenye jimbo moja kupitia vyama tofauti.
Mastaa wa filamu kutoka Nigeria Bob Manuel Udokwu na Tony One Week Muonago wanaendelea kuzungumziwa sio kwa sababu wamejiingiza kwenye siasa, bali kinachozungumziwa ni kitendo cha wao kugombea nafasi hiyo katika jimbo moja kitu  ambacho kimeanza kuvutia hisia za watu wengi.
Actors
Bob Manuel Udokwu (kushoto) na Tony One Week, waigizaji wa Nollywood waliojitosa kugombea katika Jimbo la Anambra.
Bob Manuel Udokwu anagombea kupitia chama cha APGA na Tony One Week Muonagor anagombea kwa tiketi ya ACN katika jimbo moja la Anambra, Nigeria ambapo uchaguzi mkuu wa nchi hiyo unatarajiwa kufanyika katikati ya mwaka 2015, ambapo staa mwingine wa Nollywood ambaye alitangaza kujiingiza kugombea ubunge ni Desmond Elliot.
Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza >>> twitter Insta Facebook

Msiba mwingine wa mwigizaji Bongo Movie 2014.



Mzee ManentoWiki moja  baada ya kutokea kwa msiba wa mmoja wa wasanii wa TMK Wanaume Family YP na saa chache baadaye ukatokea msiba mwingine wa aliyekuwa msanii wa maigizo na vichekesho Sherry Mwana, leo Oktoba 30 umetokea msiba mwingine Bongo Movie.
Taarifa za awali zimeanza kusambaa kupitia watu mbalimbali maarufu Tanzania ambao wameaanza kuonyesha masikito yao akiwemo msanii Bob Junior kuhusu kifo cha mzee Manento ambaye inadaiwa amefariki jana usiku.
millardayo.com inaendelelea kufuatilia kwa ukaribu kuhusiana na taarifa ya msiba huo.
Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza >>> twitter Insta Facebook

Wednesday, 29 October 2014

Zambia yapoteza Rais wa pili akiwa madarakani.




Sata II
Aliyekuwa rais wa Zambia Michael Sata amefariki usiku wa jana tarehe 28 Oktoba kutokana na ugonjwa ambao bado serikali ya nchi hiyo haijaweka wazi.
Sata (77) amefariki akiwa anatibiwa nchini Uingereza alikokuwa amelazwa kwa zaidi ya mwezi mmoja.
Rais huyo amefariki siku 4 baada ya nchi hiyo kusherehekea madhimisho ya miaka 50 tangu ipate uhuru, ambapo kutokana na kuwepo nje ya nchi akipata matibabu hakuhudhuria sherehe za maadhimisho hayo.
Rais Sata ambaye amekuwa maarufu kwa jina la ‘King Cobra‘ amekaa madarakani kwa takribani miaka 3 tangu achaguliwe kushika wadhifa huo mwaka 2011, ambapo anakuwa rais wa 2 kufariki akiwa madarakani nchini humo baada ya Levy Mwanawasa, aliyefariki mwaka 2008.

Upinzani Tanzania wapania kuing'oa CCM

Wabunge wa TZ, ambao baadhi yao wa upinzani wameungana, kuing'oa CCM.
Upinzani nchini Tanzania umetia saini makubaliano ya pamoja, kuking’oa madarakani Chama tawala.
Utiaji huo saini makubaliano ya kukishinda Chama cha Mapinduzi CCM, katika uchaguzi ujao, umefanywa na viongozi wa vyama vinne, huku tukio hilo likishuhudiwa na wafuasi wao.
Katibu Mkuu wa Chama kikuu cha upinzani CHADEMA, Dr. Willibrod Slaa ni miongoni mwa viongozi waliotia saini makubaliano hayo na amesema vyama hivyo vitasimamisha wagombea wake kwa pamoja kwenye ngazi zote za uchaguzi kuanzia serikali za mitaa mpaka ngazi ya urais.
Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim seif Sharif Hamad anasema tukio hilo la vyama kusaini makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja kwa lengo la kuing’oa CCM ni muhimu na la kihistoria.
Viongozi waliotia saini waraka huo wa makubaliano ni Freeman Mbowe Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA, Profesa Lipumba Mwenyekiti wa Chama cha wananchi CUF, Katibu Mkuu wa Chama hicho ambaye pia ni Makamu wa kwanza rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, James Mbatia Mwenyekiti NCCR Mageuzi, Mosena Nyambabe Katibu Mkuu NCCR Mageuzi, Dr Emmanuel Makaidi Mwenyekiti NLD na Tozzi Matwanga Katibu Mkuu wa NLD.

ROSE MUHANDO ADAIWA KUBWIA UNGA!

Stori: Mwandishi Wetu

HUKU mwenyewe akikanusha vikali kwamba hatumii, nyota wa muziki wa Injili Bongo, Rose Muhando bado anaandamwa na madai mazito kwamba anatumia madawa ya kulevya ‘unga’ yanayomfanya kuwa hoi kiasi cha kushindwa kutokea kwenye matamasha mbalimbali anayolipwa fedha, Risasi Jumatano linateremka nayo.
Nyota wa muziki wa Injili Bongo, Rose Muhando.
Kwa mujibu wa vyanzo, Rose anadaiwa kutumia unga kiasi kwamba, baada ya matumizi hujikuta akishindwa kufanya jambo lolote lile la…
Stori: Mwandishi Wetu
HUKU mwenyewe akikanusha vikali kwamba hatumii, nyota wa muziki wa Injili Bongo, Rose Muhando bado anaandamwa na madai mazito kwamba anatumia madawa ya kulevya ‘unga’ yanayomfanya kuwa hoi kiasi cha kushindwa kutokea kwenye matamasha mbalimbali anayolipwa fedha, Risasi Jumatano linateremka nayo.
Nyota wa muziki wa Injili Bongo, Rose Muhando.
Kwa mujibu wa vyanzo, Rose anadaiwa kutumia unga kiasi kwamba, baada ya matumizi hujikuta akishindwa kufanya jambo lolote lile la kujitafutia mkate wake wa kila siku na ndiyo maana amekuwa akikwaa skendo za kupokea fedha za shoo halafu hatokei tu!
WATOA MADAI
Hivi karibuni, akina mama watatu walifika kwenye Ofisi za Global Publisheers na kumtolea madai Rose kuhusu tuhuma zanazomwandama kwamba amekuwa akiingia mitini na fedha za watu wanaomwita kwenye matamasha ya nyimbo za Injili.
“Sisi tunavyojua, Rose anatumia madawa, wengine wanasema unga wengine wanasema sijui nini huko. Sasa akishatumia hayo madawa huwa yanamfanya awe kama amelewa na kushindwa kufanya lolote.
“Huwa anafika hatua anashinda kitandani amelala tu na hawezi kutoka, ndiyo maana mtu anaweza kumpa pesa asitokee kuimba kwa sababu anashindwa kutoka ndani kwake.
“Kwa hiyo jamani, si suala la kumwandika tu kwamba anaingia mitini na fedha za watu bali mumsaidie Rose kama kweli mnampenda, sisi wenyewe tunamwombea kwa Mungu kila siku,” alisema mama mmoja kati ya hao waliofika lakini bila kutaja majina yao.
MADAI SUGU
Madai ya kwamba, Rose anatumia madawa ni ya siku nyingi, wengi wamekuwa wakisema wana uhakika, wengine wanasema wanasikiasikia tu lakini hawana uhakika.
Mratibu wa Tamasha la Pasaka, Alex Msama.
Magazeti ya Global (Ijumaa Wikienda, Uwazi, Risasi Jumatano, Amani, Ijumaa na Risasi Jumamosi) yameshapokea madai hayo kwa muda mrefu lakini kilichokuwa kikifanyika ni kuendelea kumchunguza msanii huyo kuhusu madai hayo.
RISASI LAINGIA KAZINI KUCHUNGUZA
Kufuatia madai ya akina mama hao waliojitambulisha ni waumini wa kutoka katika kanisa moja la kilokole jijini Dar, gazeti hili liliamua kuingia kazini kufanya uchunguzi ili kubaini ukweli au uongo wa madai hayo.
WATU WA KARIBU NA ROSE
Mtu wa kwanza kumtafuta ambaye gazeti hili liliamini kwamba anaweza kujua chochote kuhusu madai hayo ni mratibu wa Tamasha la Pasaka linalofanyika kila mwaka kwenye baadhi ya mikoa, Alex Msama.
Msama: “Mimi siwezi kusema ni kweli kwani sijawahi kumwona akitumia wala sijui kama ameathirika.”
Risasi Jumatano likamsaka Katibu wa Chama cha Waimba Injili Tanzania (Chawaita), Stela Joel: “Mimi sijui, kama unasema kuna watu wamekuja ofisini kwenu na kutoa madai hayo, basi wamwombee. Lakini tutachunguza.”
MCHUNGAJI
Risasi Jumatano pia lilibahatika kuzungumza na mchungaji mmoja (jina tunalo) ambaye alisema ameshawahi kusikia taarifa hizo akamuuliza Rose lakini alimkatalia kuwa si madai ya kweli.
“Ila ninachojua mimi ni kwamba, Rose amekuwa akitumia dawa f’lani (akazitaja jina). Hizi ni dawa zinazopatikana kwa njia ya sindano. Mara nyingi mtu akiwa hajiwezi kwa maana ya kushindwa kufanya kazi anachomwa hizi zinampa nguvu.
“Niliwahi kusikia kwamba, kuna daktari mmoja katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma (akamtaja jina). Huyu ndiye aliyekuwa akimchoma sindano zenye dawa hizo Rose pale mwili unapokuwa dhaifu.
Baadhi ya madawa yaliyowahi kukamatwa.
“Ila madhara yake sasa, dawa ikiwa imekwisha mwilini, mtu anakuwa mlegevu, anahisi kizunguzungu au kulalalala, kutokwa jasho jingi na kuhisi anaumwa kiasi kwamba ukimwona unaweza kusema ni teja. Ni dawa ghali sana kwa dozi moja, nadhani ni shilingi laki sita,” alisema mchungaji huyo.
Akaongeza: “Nasikia Rose amefika mahali huwa anajichoma mwenyewe akipata dozi. Kwa hiyo kwa suala la kubwia unga nadhani alilikanusha.”

ROSE MWENYEWE SASA
Risasi Jumatano, juzi lilimpigia simu Rose lakini hakupokea hata baada ya kurudia kumpigia mara kadhaa. Likamtumia meseji na kumsomea mashitaka yote, akajibu:
“Samahani sana nawaomba mnipumzishe kuniandika...najua ni nani na kwa nini ananitenda hivyo, ni kwa sababu anataka kunitumia kwa faida yake na ni mtu hatari sana kwangu na kwa taifa zima.
“Mtu huyo anafanya haya ili kuniziba mdomo kwani najua siri zake nyingi na nzito, nashindwa kusema ataniua.”
Hata hivyo, Rose alipotakiwa kumtaja kwa jina mtu huyo ambaye Risasi Jumatano halimjui, alikataa katakata akisema anaogopa!

LORI LA MAFUTA LAANGUKA, LATEKETEA KWA MOTO DAR

Mashuhuda wakieleza yaliyotokea.
Wafanyakazi kampuni inayomiliki lori hilo ambayo bado haijafahamika, wakifanya tathmini ya hasara iliyopatikana.…
Mashuhuda wakieleza yaliyotokea.
Wafanyakazi kampuni inayomiliki lori hilo ambayo bado haijafahamika, wakifanya tathmini ya hasara iliyopatikana.
Sehemu ya matairi ilivyobaki.
Sehemu ya juu ilivyoungua.
Maofisa wa polisi wakijadiliana la  kufanya.
…Wakielekea eneo la tukio baada ya kufikia muafaka.Askari wakilinda usalama eneo la ajali.Afisa wa polisi akimpa maelekezo askari wa usalama barabarani.
Mashuhuda kila mmoja akieleza lake.
Madereva wa bodaboda wakiwa wameacha shughuli zao ili kushuhudia tukio hilo.
LORI la mafuta aina ya Scania likiwa limesheheni dizeli likitokea bandarini jijini Dar es Salaam kuelekea mikoani, liligonga tuta katika Barabara ya Morogoro, eneo la Kimara-Baruti,  likapoteza mwelekeo na kupinduka kisha kuwaka moto na kuteketea kabisa.
Wakati lori hilo likiwaka, mafuta yenye moto yalisambaa na kutaka kuunguza nyumba za jirani lakini Kikosi cha Uokoaji na Zima Moto cha Halmashauri ya Jiji, kiliwahi kufika eneo la tukio na kuudhibiti moto huo.
Tukio hilo limesababisha usumbufu mkubwa kwa magari yanayotumia njia hiyo kutokana na sehemu hiyo kupitika kwa shida.

DIAMOND KUWASHA MOTO SHEREHE ZA MIAKA 53 YA UHURU WASHINGTON DC DECEMBER 6‏


THE PRICES ARE IN EARLY BIRD SPECIAL $75 Before NOV 10.
$100 AFTER NOV 10.. THE CHOICE IS YOURs BUY NOW OR BUY LATER AND PAY MORE ...YOU GET 3 COURSE DINNER / LIVE SHOW / RED CARPET PHOTO UP / ELEGANT BALLROOM SKY VIEW SETTINGS / EXTINGUISHED PAPARAZZI / SUPERSTAR RED CARPET HOST /…

THE PRICES ARE IN EARLY BIRD SPECIAL $75 Before NOV 10.


                                    


ZIARA YA KAMATI YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA MAZINGIRA KATIKA MIGODI

Mtaalamu kutoka Mgodi wa Geita akitoa ufafanuzi kwa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira juu ya utekelezaji wa sheria ya Mazingira katika mgodi huo.  Wengine katika picha ni wajumbe wa Kamati hiyo.
Kutoka kulia, Mh. James Lembeli Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira akitoa maagizo kwa wataalamu wa mgodi wa Geita (hawapo pichani) juu ya Hifadhi…
Mtaalamu kutoka Mgodi wa Geita akitoa ufafanuzi kwa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira juu ya utekelezaji wa sheria ya Mazingira katika mgodi huo.  Wengine katika picha ni wajumbe wa Kamati hiyo.
Kutoka kulia, Mh. James Lembeli Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira akitoa maagizo kwa wataalamu wa mgodi wa Geita (hawapo pichani) juu ya Hifadhi endelevu ya Mazingira kwa mujibu wa Sheria. Wapili kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Mh. Ummy Mwalimu na wengine ni wajumbe wa Kamati hiyo.
Katika jitihada za kuhifadhi mazingira katika Mgodi wa Geita, pichani ni eneo maalumu lililotengwa kwa ajili ya utupaji wa taka zinazoharibika.
Sehemu ya Mabwawa yanayotumika katika shughuli za uzalishaji katika Mgodi wa Geita.